Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Miongozo na Utafiti
Miongozo na Utafiti

 Katika eneo la utoaji wa Miongozo, Tume inatoa huduma zifuatazo:-

  • Kuandaa Miongozo ya ajira, Mashauri ya Nidhamu, upandishwaji vyeo, ukaguzi wa Rasilimali Watu, upimaji wa utendaji kazi, maendeleo ya watumishi, uandaaji na uwasilishaji wa taarifa za utekelezaji;
  • Kutoa ufafanuzi wa Miongozo, nyaraka, taratibu na maelekezo yanayotolewa/kusambazwa na mamlaka za juu;
  • Kufanya maboresho ya Miongozo iliyozalishwa na kusambazwa kwa wadau;Kufanya uwezeshaji kwa watumishi wa umma na wadau kuhusu haki na wajibu, kanuni za maadili na mwenendo katika Utumishi wa Umma;
  • Kubainisha maeneo ya kufanya utafiti, kufanya tafiti mbalimbali za Tume, Utumishi wa Umma na kutoa ushauri kutokana na tafiti hizo;
  • Kuhamasisha Waajiri, Mamlaka ya ajira na Nidhamu kuhusu uzingatiaji wa Miongozo iliyotolewa;
  • Kuandaa na kuwasilisha taarifa za utekelezaji wa Miongozo iliyoandaliwa na kusambazwa kwa wadau; na
  • Kuwafahamisha wadau mabadiliko kuhusu Miongozo ya usimamizi wa rasilimali watu.