Majukumu ya Tume
1. Ushauri
1.1 Kumshauri Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza majukumu yake aliyopewa kwa mujibu wa Ibara ya 36 ya Katiba ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
2. Urekebu (Regulatory Function)
2.1 Kutoa Miongozo ya masuala ya Ajira na Nidhamu ambayo husaidia kuwa na tafsiri sahihi ya utekelezaji wa Sheria katika Utumishi wa Umma.
2.2 Kutoa elimu juu ya utekelezaji wa Sheria ya Utumishi wa Umma Sura ya 298 [Marejeo ya mwaka 2019].
2.3 Kufanya Ukaguzi wa masuala ya Rasilimali Watu katika Taasisi za Umma na Idara za zaSerikali.
3. Kuamua rufaa na malalamiko
Kupokea na kushughulikia rufaa na malalamiko ya Watumishi wa Umma ambao hawakuridhika na uamuzi wa Mamlaka zao za Nidhamu.