Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Idara ya Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Masuala ya Usimamizi wa Rasilimali Watu

Lengo

Kuhakikisha kuwa Sheria ya Utumishi wa Umma inazingatiwa katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma.

 

Idara inatekeleza majukumu yafuatayo-:

1. Kufuatilia uzingatiaji wa Sheria  ya Utumishi wa Umma na Kanuni zake.

2. Kusanifu, kusimamia  na kuhuisha Mfumo wa Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria katika Usimamizi wa Utumishi wa Umma.

3. Kuweka Viwango vya Uzingatiaji vya Usimamizi wa Masuala ya Kiutumishi.

4.Kufanya ukaguzi wa Kawaida na Ukaguzi Maalum wa Uzingatiaji wa Sheria  katika usimamizi wa masuala ya kiutumishi kwenye Wizara zote, Idara Zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa na Taasisi za Umma.