Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Huduma Zitolewazo

Tume inatoa huduma zifuatazo:-

  1. Kupokea na kuamua rufaa na malalamiko ya Watumishi wa Umma ambao hawakuridhika na uamuzi wa Mamlaka zao za Nidhamu na Ajira
  2. Kufanya ukaguzi Maalum na wa Kawaida wa uzingatiaji wa Sheria katika usimamizi wa masuala ya kiutumishi
  3.  Kutoa elimu kwa Wadau kuhusu uzingatiaji wa Sheria Kanuni, Taratibu na Miongozo inayosimamia Utumishi wa Umma ikiwemo haki na wajibu wa watumishi wa Umma
  4. Kuandaa na kusambaza Miongozo ya Uzingatiaji wa masuala ya kiutumishi
  5. Kuandaa Taarifa za Hali ya Utumishi wa Umma
  6. Kutoa habari kwa umma kuhusu masuala yanayohusiana na majukumu ya Tume
  7. Kutoa ushauri wa Kitaalam kuhusu uzingatiaji wa masuala ya kiutumishi kadri Mamlaka mbalimbali zitakavyohitaji
  8. Kutoa huduma nyingine kama zilivyoainishwa katika Sheria mbalimbali zilizopo