Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

TEHAMA

Lengo

Kutoa utaalam na huduma za matumizi ya TEHAMA kwa Tume.

Kitengo kinatekeleza majukumu yafuatayo-:

  1. Utekelezaji wa sera ya TEHAMA na Serikali Mtandao.
  2. Kuishauri Tume kwenye masuala yanayohusu sera zinazohusiana na utekelezaji wa TEHAMA na Serikali Mtandao.
  3. Kujenga na kuratibu Mfumo Shirikishi wa Usimamizi wa Menejimenti za Taarifa wa Tume.
  4. Kuhakikisha kuwa vifaa na program zinatunzwa kwa usahihi.
  5. Kuratibu na kuwezesha ununuzi wa program.
  6. Kuanzisha na kuratibu matumizi ya mawasiliano ya kielektroniki na kupandisha taarifa kwenye tovuti.
  7. Kuratibu usanifu wa utekelezaji na usimamizi wa program tumizi na kanzi data ya Tume.
  8. Kutoa mapendekezo kwa Tume kuhusu maeneo ya kutumia TEHAMA kama nyenzo ya kuboresha utoaji wa huduma.
  9. Kuandaa mpango mkakati, miongozo na taratibu za uendeshaji wa TEHAMA kwa kushabihiana na sera ya Taifa ya TEHAMA.
  10. Kushirikiana na UTUMISHI kuandaa viwango vya TEHAMA kwa vifaa na program.
  11. Kukusanya mahitaji ya mafunzo kuhusu TEHAMA na kuandaa mpango wa mafunzo.
  12. Kusimamia na kudhibiti vihatarishi vya miundombinu ya TEHAMA na Mifumo ya Menejimenti ya Taarifa.