Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Mipango,Tathmini na Ufuatiliaji

Lengo

Kutoa utaalamu na huduma katika Mipango, Bajeti, Ufuatiliaji na Tathmini katika Tume ya Utumishi wa Umma.

Kitengo kitatekeleza majukumu yafuatayo:

  1. Kuratibu maandalizi ya Mpango Mkakati wa muda wa kati, Mipango ya Maendeleo na Bajeti ya Tume ikiwemo  kufuatilia na kutathmini utekelezaji wake
  2. Kuandaa Taarifa za vipindi mbalimbali za utekelezaji wa miradi kadri ya muda
  3. Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Mipango ya Mwaka na Mpango Mkakati wa Muda wa Kati wa Tume
  4. Kutoa utaalamu na kusaidia michakato ya uandaaji wa Mipango na Bajeti katika Tume
  5. Kukusanya, kupitia na kuchakata takwimu zinazohitajika katika uandaaji wa mipango na maandiko mbalimbali ya bajeti
  6. Kuratibu shughuli za utafiti, tathmini ya mipango, miradi na programu zinazofanyika katika Tume
  7. Kufanya tathmini ya huduma zinazotolewa na Tume kwa wadau

Kitengo kitaongozwa na Mkurugenzi na kitaundwa na Sehemu mbili (2) kama ifuatavyo:

  1. Sehemu ya Mipango na Bajeti
  2. Sehemu ya Ufuatiliaji na Tathmini