Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

HAFLA YA KUKABIDHI VIBALI VYA UJENZI WA OFISI ZA TAASISI - DODOMA

Tume ya Utumishi wa Umma ni miongoni mwa Taasisi za Umma (55) zilizoshiriki katika hafla ya kukabidhi vibali vya ujenzi wa Ofisi za Taasisi, Dodoma iliyofanyika Ukumbi wa Hazina, Dodoma. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. George B. Simbachawene (Mb) amemkabidhi kibali cha ujenzi wa Ofisi ya Tume inayojengwa katika Mji wa Serikali Mtumba  Bw. Mathew M. Kirama, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma na katika hotuba yake Mhe. Waziri Simbachawene ( Mb) amemshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendeleza dhamira yake ya dhati ya kuhakikisha anatekeleza kwa umadhubuti mkubwa Mpango wa muda mrefu wa kuhamishia shughuli za Serikali katika Makao Makuu ya Nchi Jijini Dodoma. 

Taarifa Kwa Vyombo vya Habari

31-05-2022

TAARIFA KWA UMMA

Kurasa za Karibu

Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.