Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Ukaguzi wa Uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu katika usimamizi wa Rasilimali watu katika Utumishi wa Umma

UTANGULIZI

Tume ya Utumishi wa Umma hufanya ukaguzi wa Rasilimali Watu kwa kutumia Mamlaka iliyopewa chini ya kifungu cha 10 (1) (c) cha Sheria Na.18 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007, sheria hii imepatia mamlaka Tume kusimamia Waajiri, Mamlaka za Ajira na Nidhamu kuhakikisha kuwa wanazingatia ipasavyo Sheria, Kanuni na Taratibu katika kusimamia Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma.

Kwa mujibu wa Sheria hiyo, Tume ya Utumishi wa Umma ina mamlaka ya kufanya ukaguzi wa uzingatiaji wa Rasilimali Watu katika taasisi zote za umma nchini ikiwemo Wizara, Idara Zinazojitegemea, Sekretarieti za Mikoa, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Wakala za Serikali na Taasisi za Umma.

Tume hufanya ukaguzi kwa kutumia mfumo wa ukaguzi wa Uzingatiaji wa Rasilimali Watu wa Tume unaoitwa “Human Resource Compliance Inspection System” (HRCIS) ulioanzishwa mwaka 2005.

Mfumo huu umeandaliwa ili kuiwezesha Tume kufanya tathmini  ya uzingatiaji katika  maeneo ya  Ajira, Likizo ya mwaka, Nidhamu, OPRAS, Likizo ya ugonjwa, Upandishwaji vyeo na Usimamizi wa mafunzo.


 




 


UKAGUZI WA UZINGATIAJI WA SHERIA, KANUNI NA TARATIBU ZINAZOSIMAMIA RASILIMALI WATU KATIKA UTUMISHI WA UMMA.pdf

Taarifa Kwa Vyombo vya Habari

31-05-2022

TAARIFA KWA UMMA

Kurasa za Karibu

Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.