Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Taratibu za kupokea na kushughulikia rufaa


Tume ya Utumishi wa Umma imepewa mamlaka ya kushughulikia Rufaa za watumishi wa Umma chini ya Kifungu cha 25(1)b cha Sheria ya Utumishi wa Umma  Na.8 ya mwaka 2002 kikisomwa pamoja na Kanuni ya 60(2) ya Kanuni za Utumishi wa Umma za  mwaka 2003.

Mchakato wa Rufaa Tume ya Utumishi wa Umma hupitia katika hatua mbalimbali zifuatazo:-

  • Tume kupokea rufaa kutoka kwa watumishi walioadhibiwa  na Mamlaka zao za

    Nidhamu wakipinga maamuzi yaliyotolewa dhidi yao.

     

  • Baada ya kupokea rufaa, Tume huwaandikia Mamlaka za  Nidhamu ili walete vielelezo vinavyohusu rufaa iliyokatwa Tume (muda, vielelezo gani) ndani ya siku kumi na nne (14).

     

  • Baada ya kupokea vielelezo kutoka kwa Mamlaka ya Nidhamu, Tume huanza

    kushughulikia rufaa kwa kufanya uchambuzi wa hoja za rufaa pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa.

     

  • Rufaa ikishakamilika kuchambuliwa na Sekretarieti na kuwasilishwa mbele ya Tume kwa ajili ya maamuzi.

     

  • Baada ya maamuzi ya Tume, watumishi waliokata rufaa Tume hujulishwa uamuzi wa rufaa zao kwa barua.




Taarifa Kwa Vyombo vya Habari

31-05-2022

TAARIFA KWA UMMA

Kurasa za Karibu

Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.