Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais
Tume ya Utumishi wa Umma
1.0 UTANGULIZI
Tume ya Utumishi wa Umma imeundwa chini ya Kifungu Na. 9(1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na.18 ya mwaka 2007. Jukumu la msingi la Tume ni Kurekebu (regulate) Utumishi wa Umma nchini ili kuimarisha Utawala Bora na Uwajibikaji kwa Viongozi na Watumishi wa ngazi zote katika Utumishi wa Umma. Kwa sababu hiyo, kazi kubwa ya Tume ni kufuatilia na kusimamia Utumishi wa Umma ili kuhakikisha kuwa Utumishi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na Taratibu.
2.0 MAMLAKA YA TUME
Kifungu 10 (1) (C) cha Sheria ya Utumishi wa
Umma Na. 8 ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa na Sheria Na. 18 ya mwaka 2007
kimeipa Tume ya Utumishi wa Umma uwezo wa kutoa Miongozo na kufuatilia Uzingatiaji
wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Nyaraka katika Utumishi wa Umma.
3.0 MAANA YA MWONGOZO
·
Mwongozo
ni maelekezo maalum au Ufafanuzi wa namna ya kutekeleza jambo fulani.
·
Ni
njia ya kupitia ili kufikia mahali palipokusudiwa kwa ufanisi unaotakiwa.
·
Miongozo
inayotolewa na Tume ni maelekezo maalum kwa Waajiri, Mamlaka za Ajira na
Nidhamu, ili kutekeleza kwa ufanisi masuala yanayohusu Rasilimali Watu
kulingana na kazi au Mamlaka zao.
·
Miongozo
ya Tume ya Utumishi wa Umma iliyotolewa imesaidia sana Waajiri, Mamlaka za
Ajira na Nidhamu kutekeleza wajibu wao kama inavyotakiwa kwa hiyo kuongeza
viwango vya uzingatiaji wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Nyaraka ziliyopo.
·
Aidha,
Miongozo imesaidia Tume katika kufuatilia na kusimamia vizuri Utumishi wa Umma.
4.0 MADHUMUNI YA MWONGOZO
Madhumuni ya Mwongozo ni kuwepo kwa tafsiri
na uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa ni Sheria, Kanuni, Taratibu na
Nyaraka za masuala ya Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma.
4.1.
Faida ya Mwongozo
Zipo
faida za kuwa na Mwongozo kwa Watendaji na Wasimamizi wa masuala ya Rasilimali Watu
kwenye Utumishi wa Umma. Faida hizo ni kwamba Mwongozo:-
•
Una
jambo moja mahsusi lililotolewa maelekezo (Specific).
•
Hutumia
lugha nyepesi (simple).
•
Mpangilio
ni rahisi (systematic).
•
Hutoa
maelekezo yaliyo wazi (clear).
•
Hutoa
ufafanuzi kuhusu jambo ambalo halikuwekwa bayana kwenye Sheria, Kanuni au
Taratibu (clarity).
•
Rahisi
kutumia na kueleweka (comprehensible).
•
Rahisi
kubebeka (portable).
•
Haupotezi
muda (timekeeping).
•
Kwa
kuzingatia madhumuni na faida za Mwongozo, tunaona haja ya kuwa na Miongozo.
5.0 MIONGOZO ILIYOTOLEWA NA TUME YA UTUMISHI WA
UMMA
Tume ya Utumishi wa Umma imeweza kutoa
Miongozo Mbalimbali kama ifuatavyo:
·
Mwongozo
Kuhusu Masuala ya Ajira Katika Utumishi
wa Umma Toleo, Na.1 la mwaka 2004.
·
Mwongozo
Kuhusu Masuala ya Ajira Katika Utumishi wa Umma Toleo, Na. 2 la mwaka 2009.
·
Mwongozo
Kuhusu Mashauri ya Nidhamu na Rufaa kwa Watumishi wa Umma, Toleo Na.1 la mwaka
2005.
·
Mwongozo
kuhusu Taarifa za Kuwasilisha Tume, Toleo Na. 1 la mwaka 2005.
·
Mwongozo
Kuhusu Mashauri ya Nidhamu na Rufaa kwa Watumishi wa Umma, Toleo Na.2 la mwaka
2009.
·
Mwongozo
Kuhusu Ukaguzi wa Rasilimali Watu katika Utumishi wa Umma, Toleo Na. 1 la mwaka
2009.
·
Maelekezo
Mahsusi Kwa Mamlaka za Nidhamu na Kamati za Uchunguzi kuhusu namna ya Kuendesha
Uchunguzi wa Mashauri ya Nidhamu Na.1 ya mwaka
2008.
Tume huboresha au
huuisha miongozo kutokana na mabadiliko mbalimbali ya
Sheria, Kanuni na
Taratibu za Utumishi wa Umma zinazotolewa na Serikali,
changamoto za
utekelezaji wa masuala ya kiutumishi, mawazo ya wadau na
haja ya kuweka
bayana jambo fulani.
6.0 MAHITAJI NA
HATUA MUHIMU KATIKA KUANDAA MWONGOZO
6.1
Mahitaji
Ili
Mwongozo uandaliwe sharti kuwe na mambo yafuatayo:
•
Suala/
Jambo linalohitaji kutengenezewa Mwongozo (issue).
•
Nyenzo
Muhimu.
•
Wahusika.
6.1.1 Suala au jambo
linalohitaji kutengenezewa Mwongozo
Suala /Jambo hilo
linaweza kusababishwa na:-
•
Tafsiri
tofauti na utekelezaji unaotofautiana kuhusu jambo moja kati ya watekelezaji.
(Mamlaka za Ajira, Nidhamu au Mwajiri n.k.).
•
Kukiukwa
mara kwa mara kwa Sheria, Kanuni, Taratibu au Nyaraka.
•
Kukosekana
kwa maelezo kuhusu utekelezaji wa jambo fulani (Gaps).
6.1.2
Nyenzo Muhimu
Sera, Sheria,
Kanuni, Taratibu na Nyaraka mbalimbali zinazohusu uendeshaji wa Utumishi wa
Umma ni nyenzo muhimu zinazotumika katika kuandaa Mwongozo. Aidha, Mwongozo ni
lazima uandaliwe kwa kuzingatia nyenzo hizo zinazohusu uendeshaji wa Utumishi
wa Umma bila kukinzana au kwenda kinyume nazo.
6.1.3
Walengwa/Kundi linaloandaliwa Mwongozo
7.0
SIFA ZA MWONGOZO
Ili
Mwongozo utambulike na kukubalika ni lazima utimize sifa za kuweza kuitwa
Mwongozo. Sifa za Mwongozo ni pamoja na:
·
Kuwa
na jina/jambo linalotolewa maelekezo.
·
Kuonesha
Mamlaka iliyoutoa.
·
Kueleza
nguvu ya kisheria ya chombo kilichotayarisha Mwongozo.
·
Kuwa
na namba na mwaka wa kutolewa.
·
Kuwa
na dibaji.
·
Kuainisha
wahusika wa Mwongozo huo.
·
Kuwa
na saini ya mwenye mamlaka.
·
Kutaja
tarehe ya kuanza kutumika.
·
Kuwa
na utangulizi.
·
Kueleza
madhumuni ya Mwongozo huo.
·
Kutoa
maelekezo kwa ufasaha.
·
Kuwa
na viambatisho.
8.0 HITIMISHO
Vyombo vilivyopewa jukumu la kusimamia rasilimali watu
vina wajibu wa kuona kuwa Sheria, Kanuni na Taratibu zinazingatiwa kwa viwango
vya hali ya juu katika kuendesha Utumishi wa Umma. Aidha, ni wajibu wa vyombo
hivyo kuona umuhimu wa kuwasaidia watendaji kwa kutoa Miongozo ili
kuhakikisha uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu katika kuimarisha Utawala Bora.
Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.