Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

MRADI WA UJENZI WA JENGO LA OFISI YA TUME YA UTUMISHI WA UMMA UTAKAMILIKA KWA WAKATI

Mhandisi Kelvin Chuma kutoka  Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) leo ameongoza kikao cha "site meeting" kuhusu mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Tume ya Utumishi wa Umma unaoendelea katika mji wa Serikali Mtumba, Dodoma. Kikao kimefanyika eneo la mradi mji wa Serikali, Mtumba ambapo pamoja na mambo mengine mkandarasi CRJE (EA) LTD amewasilisha taarifa ya utekelezaji na hatua iliyofikiwa katika mradi huu.
Kaimu Katibu wa Tume, Bw. John Mbisso ameshiriki katika kikao hicho na ametembelea  mradi kuona kazi  inayoendelea kufanyika na hatua iliyofikiwa. 

Kurasa za Karibu

Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.