Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Rais

Tume ya Utumishi wa Umma

Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma wanatembelea Zanzibar

Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji Mstaafu Mhe. Hamisa H. Kalombola na Makamishna wa Tume leo tarehe 14/08/2023 wameanza ziara ya siku tatu kutembelea Zanzibar ambapo wanatarajia kukutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Zanzibar Mhe. Haroun Ali Suleiman, Ofisini kwake Mazizini. Katika ziara hii Makamishna wa Tume watatembelea pia Kamisheni ya Utumishi wa Umma Zanzibar, Tume ya Kurekebisha Sheria Zanzibar na  Tume ya Utumishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Mwenyekiti wa Tume katika ziara hii atakuwa  na Makamishna, Mhe. Khadija A.M. Mbarak, Mhe. Balozi John M. Haule. Mhe. Immaculate P. Ngwale, Mhe. Balozi Adadi M. Rajabu, Mhe. Susan P. Mlawi na Mhe. Nassor N. Mnambila pamoja na Bw. Mathew M. Kirama, Katibu wa Tume.  

Kurasa za Karibu

Hakimiliki © 2014. Tume ya Utumishi wa Umma. Haki zote zimehifadhiwa.